By Jamal Maherea


UTANGULIZI: #
Kampeni ya kumsaidia mtoto riziki, mwenye ulemavu wa viungo, ilianzishwa tarehe 14 Oktoba 2024 kwa lengo la kumuwezesha kupata mahitaji yake muhimu. Kampeni hii iliendeshwa kwa ushirikiano wadau walioguswa na changamoto anazokabiliana nazo mtoto riziki ikiwa ni pamoja na watu binafsi pamoja na kampuni ya Yammy Yami diapers.
MAFANIKIO YA KAMPENI: #

Kampeni ilifanikiwa kwa kiasi kikubwa, ambapo ilikusanya pesa taslim, kiti mwendo kimoja pamoja na diapers 400 kutoka Yammy Yami diapers amabo wamekuwa na mchango mkubwa katika kufanikisha kampeni hii.Â

Kwa msaada wa kampeni hii, hali ya maisha ya Riziki yataendelea kuboreka. Yeye na familia yake wameonyesha furaha kubwa kutokana na msaada wa hali na mali waliopatiwa.
SHUKRANI: #
Tunapenda kutoa shukrani za dhati kwa wote waliochangia kampeni hii kwa hali na mali; bila msaada wenu, mafanikio haya yasingewezekana. Shukrani za kipekee kabisa tunazielekeza kwa Yammy Yami diapers kwa kukubali kushrikiana na MBS TRINITY CARE kufanikisha kampeni.
HITIMISHO: #
Kampeni ya kumsaidia mtoto riziki imedhihirisha jinsi ushirikiano wa jamii unavyoweza kubadilisha maisha ya watu. Tukiwa na moyo wa upendo na msaada wa pamoja, tunaweza kusaidia watoto wengi zaidi wenye ulemavu kuishi maisha yenye furaha na matumaini. Tunawasihi kama wanajamii, tuendelee kuungana kwa ajili ya kuwasaidia watoto na wanajamii kwa ujumla wenye mahitaji maalum.
Kindness is the Greatest!