MAZOEZI KWA AFYA

By Debora K. Mwangosi Mazoezi yanamaanisha shughuli za kimwili zinazofanywa na mtu ili kuboresha au kudumisha afya, nguvu, na ustawi wa mwili. Hii inaweza kujumuisha aina mbalimbali za shughuli kama vile kukimbia, kutembea, kuogelea, kufanya mazoezi ya nguvu, au michezo ya aina mbalimbali. Mazoezi yanaweza kuwa ya kawaida au maalum kulingana na malengo ya mtu, kama vile kupunguza uzito, kujenga misuli, au kuboresha stamina. Kwa ujumla, mazoezi yana lengo la kuongeza ufanisi wa mwili na kuboresha hali ya kiafya. Watu wengi wanakabiliwa na changamoto za kutofanya mazoezi kwa sababu mbalimbali, 1.Ukosefu wa Muda: Katika maisha ya kisasa, watu mara nyingi wanashughulika na kazi, familia, na majukumu mengine, hivyo hawana muda wa kutosha wa kujitenga kwa ajili ya mazoezi. Na hii yote inatokana na mabadiliko ya mfumo wa maisha. 2. Uchovu: Baada ya siku ndefu ya kazi au shughuli nyingine, wengi wanahisi uchovu na wanapendelea kupumzika badala ya kufanya mazoezi. Kutona na gharama za maisha watu wanaamua kufanya kazi sana zaidi ya muda  uliopangwa. 3.Mazingira: Ukosefu wa maeneo bora ya kufanya mazoezi, kama viwanja vya michezo au Ukumbi maalumu wa mazoezi yaani ‘gym’, kunaweza kuwa kikwazo. Vilevile, hali mbaya ya hewa inaweza kuathiri watu kufanya mazoezi nje. Lakini dunia ya sasa imeendelea sana na kupelekea hata kuwepo kwa maeneo ya mazoezi. 4.Mabadiliko ya Mtindo wa Maisha: Teknolojia na urahisi wa maisha ya kisasa yamefanya watu wengi kukaa zaidi kwenye nafasi zao, na kupunguza shughuli za mwili. Na hii ni tatizo kwa watu wengi sana kuendekeza mtindo wa maisha wa sasa na kusahau kuangalia afya. 5. Afya: Watu wenye matatizo ya kiafya au maumivu ya mwili wanaweza kukumbana na changamoto za kufanya mazoezi, na hii inaweza kuwa sababu ya kutokufanya. Kuhakikisha kuwa mazoezi yanakuwa sehemu ya maisha ya kila siku kunaweza kusaidia kupunguza hizi changamoto, kama vile kuweka malengo ya ukweli, kupata mwenzako wa kufanya mazoezi, au kujitengea muda maalum kwa ajili ya shughuli za mwili. Mazoezi ni sehemu muhimu ya maisha ya binadamu, kwani yanachangia afya bora na ustawi wa mwili na akili. Hapa kuna baadhi ya faida za mazoezi: Afya ya Mwili: Mazoezi husaidia kuimarisha mifupa na misuli, kuongeza ufanisi wa moyo na mapafu, na kuboresha mzunguko wa damu. Hii inasaidia kupunguza hatari ya magonjwa kama kisukari, shinikizo la damu, na magonjwa ya moyo. Kupunguza Uzito: Kwa kufanya mazoezi mara kwa mara, mtu anaweza kudhibiti uzito wake, kwani mazoezi yanasaidia kuchoma kalori na kuongeza kiwango cha kimetaboliki. Na watu wengi wanakumbuka kufanya mazoezi baada tu ya kuona kuwa mwili ushaongezeka na kuuthibiti ni changamoto. Afya ya Akili: Mazoezi yanaweza kusaidia kupunguza msongo wa mawazo, wasiwasi, na unyongovu. Hufanya ubongo kutolewa kemikali kama vile endorphins, ambazo huongeza hisia za furaha. Ufanisi wa Kazi: Watu wanaofanya mazoezi mara kwa mara huwa na nguvu zaidi na wanakuwa na uwezo mzuri na kufanya kazi kwa ufanisi zaidi; kwasababu mwili unakuwa na nguvu hamna uchovu au uzembe wowote. Kuimarisha Mfumo wa Kinga: Mazoezi yanaweza kusaidia kuimarisha mfumo wa kinga wa mwili, hivyo kupunguza hatari ya kuugua magonjwa mbalimbali. Kuongeza Uwezo wa Kijamii: Kushiriki katika shughuli za mazoezi kama vile michezo ya kikundi kunaweza kuimarisha uhusiano wa kijamii na kujenga urafiki mpya. Ili kufaidika na mazoezi, ni muhimu kufanya mara kwa mara; angalau dakika 150 za mazoezi ya wastani kwa wiki, kama inavyoshauriwa na wataalamu wa afya. Mazoezi yanaweza kuwa ya aina mbalimbali kama vile kutembea, kukimbia, kuogelea, au kufanya mazoezi ya nguvu. Muhimu ni kuchagua aina ya mazoezi yanayofaa na yanayovutia ili kuweza kuendelea nayo kwa muda mrefu. Kwa maisha ya sasa ya utandawazi watu wamekuwa wakijasahau sana katika swala zima la ufanyaji wa mazoezi. Magonjwa yamekuwa mengi sana kutokana na mtindo mpya wa Maisha. Vijana wanapoteza ufanisi wao wa kufanya kazi kutokana na uzembe wa kutunza afya zao. Vijana lazima tukumbuka hatuwezi piga hatua mbele bila kujali afya ya miili yetu, bila hivyo ni kama kutwanga maji kwenye kinu. Ni rahisi kupata mbinu za kupata pesa lakini ni changamoto sana kupata mbinu kama afya ikiwa tete maana kila kitu kuazia akili yako, mwili vinakuwa vimedhoofika. Unaweza jiuliza kwa nini nazungumza sana na vijana, jibu ni kwamba, hawa ndio nguvu kazi ya jamii na taifa kwa ujumla. Malengo, ndoto au maono tuliyobeba bila kuzingatia mazoezi kwa afya ni kazi bure. Hivyo nahitimisha kwa kuwasihi vijana wezangu na jamii kwa ujumla ‘AFYA NI MTAJI WA KESHO’.

MAZOEZI KWA AFYA Read Post »

ESSENTIAL TIPS FOR A BALANCED LIFESTYLE

By Maureen C. Minanago Maintaining a healthy body is fundamental to leading a fulfilling and energetic life. It encompasses not just physical fitness but also a balanced approach to nutrition, mental well-being, and overall lifestyle. Here’s a guide to help you achieve and sustain optimal health through practical and achievable steps. 1. Balanced Nutrition A well-rounded diet is crucial for maintaining good health. Focus on: 2. Regular Physical Activity Exercise is key to maintaining physical health. Aim for: 3. Adequate Sleep Quality sleep is vital for overall health. To improve your sleep: 4. Mental Well-being A healthy mind is integral to a healthy body. Support your mental health by: 5. Preventive Health Care Regular health check-ups and screenings are crucial for early detection and prevention of diseases: 6. Healthy Habits Incorporate the following habits into your daily routine to support overall health: Therefore, maintaining a healthy body involves a holistic approach that integrates balanced nutrition, regular exercise, adequate sleep, mental well-being, and preventive care. By adopting these practices, you can enhance your overall quality of life, boost your energy levels, and reduce the risk of chronic diseases. Remember, consistency is key, and small, gradual changes can lead to lasting improvements in your health. Prioritize your well-being today, and your future self will thank you for it.

ESSENTIAL TIPS FOR A BALANCED LIFESTYLE Read Post »

MAZOEZI SI HAKIKA YA AFYA NJEMA

By Maureen C. Minanago Mazoezi ni muhimu kwa kukuweka mwenye nguvu muda wote lakini maisha unavyoyaishi pia yanachangia katika kukufanya mwenye furaha, mchangamfu na mwenye afya njema. Dr. Denis Nturibi anasema kuna vitu vitatu ambavyo binadamu wote tunapaswa kuvifuata ili kuwa na afya njema. Mazoezi ni sahihi kuyafanya lakini muundo wa maisha (lifestyle) yetu unamchango mkubwa pia. 1. Kula sahihi. Tunapaswa kupata lishe bora kwa maana kwamba tuachane na vyakula ambavyo vinanenepesha hasa vyenye mafuta mengi na sukari nyingi. Tusile sana yaani tule kwa kiwango na kwa muda tu. Kuna watu wanakula kwa siku hata zaidi ya mara nne. Kila unachoona unataka uonje. Basi tujitahidi kujiwekea mipaka yaani nini kiliwe na kwa muda na kiwango gani, Bila kusahau maji ya kunywa (angalau lita moja kwa siku). 2. Pumzika na lala. Tunafanya kazi kupata hela, sawa kabisa. Hata Mungu anatuambia tufanye kazi na ametuweka duniani hasa kufanya kazi bila hivyo hatupati kula. Lakini kila kitu kiwe kwa kiasi. Pata muda wa kutosha wa kupumzika. Kazi nyingi zinatufanya tutumie akili sana katika kufikiria, kusuluhisha na kudadavua mambo kitu ambacho huchosha sana akili na mwili pia.  Lala masaa yanayotakiwa (8-10). Usitumie muda mwingi kuangalia luninga ukakesha asubuhi unaelekea darasani au ofisini. Usisome masaa tisa ukalala kwa saa moja au kuvusha kabisa halafu uingie kufanya mtihani. Pumzika  na lala ili akili pia ipumzike na mwili kwa ujumla. 3. Shughuli za kimwili. Mazoezi ya viungo ni muhimu katika kukufanya mwepesi. Kimbia taratibu (jogging) au tembea kwa mwendo wa haraka kwa umbali kidogo kila siku au walau mara mbili kwa wiki. Hii itakusaidia kukupa pumzi nzuri. Kwa wale waimbaji, sauti yako itapunguza kuhema hema.Kwahiyo, Dr. Dennis anaeleza vizuri kuwa, mazoezi pekee si afya, lishe na kupumzika pamoja na kulala vinasaidia kwa afya bora. Unaweza kuwa na mwili mdogo na wenye nguvu sababu ya mazoezi lakini kama unakunywa pombe sana au unavuta sigara utakuwa na nguvu bila afya njema.Jitengenezee mazingira mzuri ya kuwa na afya muda wote kwani afya njema ndio kila kitu.

MAZOEZI SI HAKIKA YA AFYA NJEMA Read Post »

Tumbo la kuhara

By Maureen C. Minanago HUDUMA YA KWANZA Ni matumaini yangu hakuna mtu ambaye hajawahi kuumwa tumbo hata siku moja toka azaliwe. Lakini leo naongelea kuvurugwa kwa tumbo. Yawezekana ukawa umepata chakula mchnaganyiko ama vinywaji tofauti ambavyo vikasababisha kuvurugika kwa tumbo. Inawezekana ukawa umetoka sehemu moja kwenda nyingine yaani kubadilika kwa mazingira, hivyo kuhisi umevurugika tumbo. Lakini pia yawezekana ukawa unahofu sana kutokana na kusubiri matokeo fulani kama ya mtihani kimasomo ama majibu ya daktari ama ya usaili wa kazi. Yote haya na mengine mengi husababisha kuvurugika kwa tumbo na mara nyingi kupelekea kutaka kuhara (kuharisha). Mvurugiko huu wa tumbo humfanya mtu kukosa raha na hasa pale anapokuwa nje ya mazingira ya nyumbani ama sehemu iliyo karibu na huduma ya choo. Unachoweza kufanya ni kutafuta dawa ya kuzuia kuharisha kwenye maduka ya dawa yaliyoko karibu na wewe. LAKINI, si mara zote itawezekana kuwa hivyo, basi nini kifanyike unapokosa dawa hizo? Ukiwa nyumbani, chukua sukari na chumvi kisha chota chumvi kijiko kidogo cha chai nusu uweke kwenye kikombe na kiasi hicho hicho chota sukari uweke. Baada ya hapo changanya na maji kidogo sana ili kuepuka kupoteza ladha ya ukali dawa hiyo. Kwa kuwa uliweka kijiko kidogo nusu basi maji yaweke kiwango cha vijiko vikubwa vya kulia chakula vitano au sita. Koroga mchanganyiko wa chumvi na sukari kisha kunywa yote bila kuisikilizia. Tumbo litakata maumivu na dalili za kuhara mara moja. Na kama uliishaanza kuhara basi hali hiyo itaisha. Ukiwa nje ya mazingira ya nyumbani na hujapata msaada wowote wa chumvi na sukari ama dawa, basi tafuta maji safi ya kunywa walau lita moja kisha vuta pumzi ndani na nje kwa nguvu kwa muda wa dakika tatu mpaka tano. 

Tumbo la kuhara Read Post »

EMPOWERING SECONDARY SCHOOL GIRLS IN DODOMA REGION THROUGH SANITARY PAD DISTRIBUTION

By Happiness Silivester Masatu Empowering secondary school girls in Dodoma Region through sanitary pad distribution is a crucial initiative aimed at addressing menstrual hygiene management (MHM) challenges and promoting girls’ education. Menstrual hygiene remains a significant barrier to girls’ education in many parts of the world, including Dodoma Region, where access to sanitary pads is limited, leading to absenteeism and dropouts among girls. This proposal outlines a comprehensive plan to distribute sanitary pads to secondary school girls in Dodoma Region, thereby empowering them to stay in school and pursue their education. Various initiatives have been implemented by governmental bodies and other relevant stakeholders, such as the Campaign for Female Education (CAMFED), African Medical and Research Foundation (AMREF), Tanzania Youth Alliance (TAYOA), Population Services International (PSI), and FEMINA, to enhancing menstrual hygiene management for girl students in Tanzania. These programs encompass activities such as raising awareness among female students regarding the management of menstrual hygiene, delivering reproductive health education, and supplying sanitary pads to adolescent females. Despite the implementation of many efforts, Tanzania exhibits a subpar performance in terms of knowledge, attitude, and behavior regarding menstrual hygiene management, with discernible disparities observed between rural and urban regions. This is due to insufficient provision of hygiene products, access to clean water, sanitation facilities, and particularly within educational institutions, which have a detrimental effect on the management of menstruation among adolescent girls. Conduct Needs Assessment of six Schools in Dodoma region: Begin with a comprehensive needs assessment to understand the specific challenges faced by girls regarding menstrual hygiene management in Dodoma Region. Below is a table of findings from a research done in year 2023. Proposal : Empowering Secondary School Girls in Dodoma Region Through Sanitary  Pad Distribution               Result Areas Unit # Unit  Unit Rate Unit # Unit  Amount (TZS) Activity 1.1 Conduct  a comprehensive needs assessment to understand the specific challenges faced by girls regarding menstrual hygiene management in Dodoma Region ParticipantsAllowance  Pts           5   100,000.00 days 6                    3,000,000.00 Meals and refreshments  Pts           5     20,000.00 days 6                      600,000.00 Stationaries  Pts         10       4,000.00 days 6                      240,000.00 Contigency  Pts           1   500,000.00 days 1                      500,000.00 Car Hire  Pts           1   300,000.00 days 6                    1,800,000.00 Sub total                              6,140,000.00                  Activity 2.1 Distribution of Sanitary Pads to selected Secondary School in Dodoma region Procurement of Sanitary pads Pts   3,035            3,000     days      12                   109,260,000.00 Transport and logistics BOX       80            5,000     days        1                         400,000.00     Car Hire pts         1         300,000     days        6                       1,800,000.00     Hygene Education  workshop students         5         100,000     days        6                       3,000,000.00     Meals and refreshments Pst       10          30,000     days        6                       1,800,000.00    Contigency Pst         1         500,000     days        1                         500,000.00    Media people Pst         5          50,000     days        6                       1,500,000.00    Facilitation fee pts         1         200,000     days        6                       1,200,000.00   Photer & video pts         2         200,000     days        6                       2,400,000.00 Facilitation transport pts         1         100,000     days        6                         600,000.00 Subtotal                          122,460,000.00               Moniotoring and Evaluation:monitoring and evaluation framework to track the distribution process’s effectiveness and impact on girls’ attendance, academic performance, and overall well-being Participanta Allowance Pts           5   100,000.00 days 6                    3,000,000.00 Venue venue           1   200,000.00 days 2                      400,000.00 Stationery Pts         10       4,000.00 days 2                        80,000.00 Contogency Pts           1   500,000.00 days 1                      500,000.00         Car Hire Pts           1   300,000.00 days 6                    1,800,000.00 Sub-total                              5,780,000.00                                                                                                                                                                                                                                                                                     Sub total Monitoring Activities                          134,380,000.00               GRAND TOTAL                134,380,000.00 Hence, empowering secondary school girls in Dodoma Region through pad distribution is a vital step towards promoting gender equality in education and improving girls’ overall well-being. By providing access to sanitary pads and menstrual hygiene education, we can empower girls to stay in school, achieve their academic potential, and contribute positively to their communities. This proposal outlines a strategic plan to implement this initiative effectively, but its success depends on collaborative efforts and support from all stakeholders involved. Support girls, support mankind, at MBS we say, Kindness is the Greatest!

EMPOWERING SECONDARY SCHOOL GIRLS IN DODOMA REGION THROUGH SANITARY PAD DISTRIBUTION Read Post »

“Watu wenye ulemavu wanahaki ya usawa na kuheshimiwa”.

By Maureen C. Minanago Kuna ulemavu wa aina mbali mbali. Machache yajulikanayo ni kushindwa kutembea kushindwa kutumia mikono, kutoona vizuri ama kutoona kabisa, ulimi kuwa mzito hivyo kushindwa kuongea, kutosikia (kiziwi), mifupa kujikunja na kusababisha matege pamoja na kukosa melanin itengenezayo rangi ya ngozi (albino). Watu wenye ulemavu wanapaswa kujijali pia, wanapaswa kupata lishe iliyo bora kabisa ili kujikinga na maradhi. Hawapaswi kujihurumia na kujitenga, bali kuwa na jamii yao, hivyo kuwa na afya ya mwili na akili na kuwa na amani. Dkt. Abdallah Possi ni mtu mwenye albinism lakini anatumia fursa ya kuwa kiongozi kuielimisha jamii zaidi juu ya watu wenye ulemavu na kuwaasa waachane na mitazamo potofu ya kulionea kundi hilo.  Dkt Possi anasema, ”Kila mtu ni sawa lakini usawa huo uzingatie mtu na mtu; yaani, kila mtu aheshimiwe na kusikilizwa kulingana na nafasi ama hali aliyonayo”. Kundi la watu wenye walemavu limeonekana kuachwa nyuma kwani ni wachache na watu wengi wameonekana kuwaacha walio wachache na wale wachache wanajiona sio wa kawaida.  Amesema, ili kutibu historia ya muda mrefu ya watu wenye ulemavu kuachwa nyuma, haipaswi kuwepo kwa mtazamo wa upendeleo bali wachangamke ili kujitoa katika kundi walilomo kama; ilivyokuwa katika swala la wanawake.

“Watu wenye ulemavu wanahaki ya usawa na kuheshimiwa”. Read Post »

AFYA ni nini?

By Maureen C. Minanago Afya ni hali ya kutokuwa na ugonjwa au kidonda. Afya ni hali ya kuwa na amani ya roho. Afya ni ubora wa akili, mwili na nafsi. Afya hutegemea vitu hivi vitatu ili kuwa hai na salama: Akili, Mwili, Nafsi. Akili ni utashi tuliopewa na Mwenyezi Mungu katika kung’amua mambo ulimwenguni. Akili hujumuisha uelewa, ufikiri, uamuzi na utendaji wa mambo. Hakuna awezaye kutafsiri akili yetu ila matendo yetu yanaweza kumfanya mtu aone flani yuko vipi; nayo bado itakuwa mtazamo wake sababu tunatofautiana kufikiri pia.  Binadamu hutumia akili kila siku na kila wakati ili kuelewa, kufikiri, kuamua na kuhakikisha tunatimiza jambo. Kwa maana hiyo, tunapaswa kuipumzisha “PUMZISHA AKILI”. Akili ikichoka mwili nao huchoka na hutafanya chochote sababu haitakuwa na uwezo mzuri kutenda. Lala au oga au ogelea au sikiliza mziki au chochote ukipendacho ambacho hakitakufanya utumie nguvu ya akili. Mwili ni muundo wote wa binaadam. Ni maumbile ya mtu. Mwili huhusisha yote yaliyotengeneza “mtu” mfano viungo kama miguu, mikono n.k, Maji kama mate, damu n.k, na vingine kama mishipa kucha na nywele. Tunapaswa kujipenda kwa kula vizuri, kulala vizuri na pazuri, kuvaa vizuri na kujijali muda wote kwa kuuweka mwili salama mfano kwa kupiga mswaki baada ya kula, kuosha nywele mara kwa mara, kukata na kusafisha kucha, kuoga, na kuvaa nguo safi. Pia tujiepushe na hatari, ugomvi na makwazo kwa faida ya mioyo yetu.  Ukitembea sana juani pata kivuli unywe na maji. Penye baridi uvike mwili wako kwa sweta ama nguo nzito. Ukiumia au kuumwa pata matibabu sahihi kwa kwenda hospitalini. Jipende, Ujali mwili wako. Tukifanya hivyo miili yetu itakuwa salama.  Nafsi ni roho yenye kuleta imani ndani yetu. Sisi huamini vitu mbali mbali kwa msaada wa nafsi. Lakini yote heri kama tutaamini vitu vyenye kujenga na sio kubomoa. Nafsi pia hutofautiana ya mtu na mwingine ndio maana tukawa tofauti japo chimbuko letu kiuumbaji ni moja.  Nafsi nayo huhitaji utulivu ili kuupa mwili na akili nguvu za kuishi kwa afya. Pata muda wa kutulia ukiongea na WEWE kujua nini waweza fanya LAKINI, mshirikishe MUUMBA wako kwa yote kupata amani uitakayo moyoni na kwa wakuzungukao. Hivyo basi, jipe likizo au omba likizo. Tembelea sehemu mbali mbali za starehe au vivutio kutuliza mwili, akili na roho pia. Ongea vizuri na watu, cheka, tabasamu hata kama umeumizwa. Inasaidia sana.  Afya ya vitu vyote vitatu ni muhimu katika kukuweka mwenye nguvu na furaha.  Jali afya yako!

AFYA ni nini? Read Post »

Urefu wa Kupindukia

By Maureen C. Minanago Wewe ni mrefu? Ni mara ngapi umekutana na watu warefu? Ni nini kinafanya mtu awe mrefu? Fuatilia….. Wanabiolojia wa molekuli (molecular biologists) wanaeleza kuwa tofauti ya urefu wa mtu na mtu kwa asilimia 60 mpaka 80 unatokana na maumbile huku asilimia 20 mpaka 40 unatokana na sababu za mazingira hasa lishe.  Urefu wa maumbile sana sana ni ule unaorithiwa hasa kutoka kwa mwanafamilia ama ndugu wa karibu. Kila mmoja anahomoni za ukuaji (somatotropin) ambazo zinamsababisha kurefuka haraka ama taratibu. Utofauti huu ndio unaoleta utofauti katika urefu wa mtu na mtu.Hizi homoni zina protini 191 zenye amino acid na uzito wa daltoni 22,124; na huzalishwa kwenye glandi iitwayo pituitary ambayo husambaza homini hizo mwilini kwa ajili ya ukuaji mara baada ya uzalishaji wake. Wengi wetu tutakumbuka msemo wa wazazi kwa watoto wao wa “lala ukue” kama kumuhamasisha aende kulala hasa wakati wa mchana ambapo watoto wengi hupenda kuutumia kucheza. Inawezekana baadhi wa wazazi wanautumia kama mazoea lakini msemo huo unaukweli ndani yake. Usambazaji wa homoni huchukua muda wa masaa matatu hadi matano lakini mtu hurefuka haraka ndani ya lisaa limoja tu akiwa amelala usingizi mzito. Hivyo ukuaji kutokea mara baada ya usambazaji wa homoni zinazohusika na ukuaji. Zikisambaa haraka na kwa wingi ndivyo mtu akuavyo mrefu zaidi kwa kipindi kifupi tu. Homoni hizi hufanya kazi kwa ufanisi zaidi kwa watoto na vijana ambao wako katika kipindi cha ukuaji, na si kwa mtu mzima. Wazazi tuwashauri watoto wetu kupata usingizi wa kutosha ili kumsaidia kukua haraka. Yamkini hawa ni wapenzi, pamoja na kuwepo kwa tofauti zao kiurefu bado wanaonekana kupendana. (picha kushoto) Hawa nao ni marafiki, wao huchweza pamoja mpira wa kikapu. Wanaonekana kuwa wenye furaha sana ukiweka kando ukweli kuwa wamepishana sana urefu. (picha chini kulia) Hivyo, kama wewe ni mrefu kuzidi wenzako usijione wa tofauti sana, kaa nao, cheza nao, furahi pamoja nao na wala usijitenge kwani furaha yako ni furaha ya jamii nzima.Na kama wewe si mrefu usijishangae pia na wala usimtenge aliye mrefu zaidi yako. Kinachofanya mtu awe mkubwa zaidi au mdogo zaidi ni sehemu ya mbele ya glandi ya pituitary iitwayo ‘anterior pituitary’. Ikifanya kazi kupita kiwango humfanya mtu kuwa mrefu mno yaani ‘giant’ na vile vile inapofanya kazi chini ya kiwango basi mtu huwa mfupi zaidi yaani ‘dwarf’. Ewe kijana, unataka kuwa mrefu? Nawe mzazi, unataka mwanao arefuke vizuri? basi kama uko kwenye umri wa ukuaji bado unayo nafasi. Epukana na vyakula vyenye mafuta na sukari nyingi (junk food). Pata lishe iliyobora kuisaidia glandi inayohusika na homoni za ukuaji kufanya kazi sahihi katika mwili wako. Hakikisha unapata usingizi wa kutosha ili kurahishisha somatotropin (homoni za ukuaji) kufanya mzunguko vizuri katika mfumo wake. Kunywa maziwa ili upate calcium itakayokuimarishia mifupa yako. Urefu ukiambatana na mifupa legevu unaweza kupata matege lakini ukipata calcium basi unakuwa imara muda wote. Kula vyakula vyenye amino acid mfano samaki, mayai, mboga mboga kama mabilinganya na matunda kama karoti matikiti na maepo.

Urefu wa Kupindukia Read Post »

Fahamu Faida za Maziwa Mtindi

By Maureen C. Minanago Maziwa mtindi yanavirutubisho vingi sana vinavyopendkezwa kuwa na faida nyingi katika mwili wa binadamu. Ni lini mara yako ya mwisho kupata maziwa mtindi? Pata kama chakula ama baada ya chakula ama kabla ya chakula, yatakusaidia. Soma faida zake hapa. Kabla ya kuzifahamu faida ya maziwa mtindi kwanza tuone virutubisho vichache vinavyopatikana ndani yake. Mtindi una calcium, phosphous, riboflavin (vitamin B2), iodine, vitamin B12. panantothenic acid (vitamin B5) zinc, potassium pamoja na molybdenum. Mbali na virutubisho hivyo, maziwa mtindi pia yana wadudu ambao ni “bakteria hai” wenye umuhimu mwilini kiafya.  Kuna homoni (cortisol) sehemu ya katikati ya tumbo na kiuno ambayo inakazi ya kuamuru ubongo kuongeza mafuta chini ya tumbo hivyo kusababisha kitambi.  Maziwa mtindi husaidia kupunguza ama kuondoa kabisa kitambi Kwa asilimia 82; kwa msaada wa madini ya calcium yaliko kwenye mtindi ambayo hupunguza homoni inayoamuru mafuta kwenda chini ya kiuno. Ni vema kunywa kutumia maziwa mtindi mara moja moja hasa wakati wa jioni unapokuwa umepumzika yaani baada ya shughuli zako. Pata mtindi ukiambatanisha na maji mengi ili kurahisisha mfumo wa upatikanaji wa maji mwilini. Mtindi huufanya mwili kuwa na maji muda wote yaani usiwe mkavu. Faida zingine ni pamoja na:  Kurefusha Maisha Kwani yanauwezo wa kupambana na magonjwa.Ni kinga kwa kina mama kwani inakinga dhidi ya maradhi ya kuambukiza ukeni (vaginal infections).Ni kinga ya mwili kwani inapambana na magonjwa kama saratani mfano saratani ya utumbo.Kuondoa lehemu (cholesterol) mbaya mwilini hilo kumuepusha mtu na tatizo la shinikizo la damu.Kupunguza uzito kwa asilimia 22 kwani yanapunguza mafuta mwilini.Yanasaidia kukupa seli za misuli yako kupitia virutubisho vya protini.Yanasaidia kuupa mwili nguvu kupitia virutubisho vya wanga.Chonde: Usitumie maziwa ya mtindi yatokanayo  na maziwa ya unga kwani utakosa ule uchachu na bakteria hai wenye umuhimu mwilini, hivyo kukosa virutubisho mwilini.  Unaweza pata maziwa mtindi kama mboga ukala na ugali, unaweza kuyanywa yenyewe kama chakula, unaweza kuyanywa na kitafunwa kama biskuti, mkate au maandazi. Wengi wetu hupenda kupunguza miili kwa mazoezi lakini jambo kubwa tunalosahau ni lishe bora na / mlo kamili. Ukifanya mazoezi ukaendelea kula vyakula vyenye mafuta kwa wingi, hutakuwa umepunguza tatizo. Fanya mazoezi kisha pata maziwa mtindi ujionee tofauti. 

Fahamu Faida za Maziwa Mtindi Read Post »

Scroll to Top